Jinsi ya Ku-apply Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) – 2025/2026
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ni moja ya vyuo vikuu vikubwa na vinavyoongoza Tanzania katika kutoa elimu ya juu bora. Kila mwaka, UDOM hupokea maelfu ya maombi kutoka kwa wanafunzi wanaotamani kujiunga na kozi mbalimbali ngazi ya Shahada, Astashahada (Diploma), na Cheti. Makala hii itakuongoza hatua kwa hatua jinsi ya kutuma maombi ya kujiunga na UDOM kwa njia ya mtandao.
1. Kitu cha Kwanza: Kuweka Tayari Mahitaji Muhimu
Kabla ya kuanza mchakato wa ku-apply, hakikisha unayo yafuatayo:
- Nakala za vyeti vya elimu ya sekondari (CSEE), kidato cha sita (ACSEE), au vyeti vya diploma/cheti (kutegemea na kozi unayoomba).
- Namba ya mtihani (ya NECTA au NACTE)
- Barua pepe inayofanya kazi
- Namba ya simu ya mkononi iliyo hai
- Passportsize photo (kama itahitajika)
- Ada ya maombi (Application fee), inayolipwa kwa njia ya simu au benki.
2. Tembelea Tovuti Rasmi ya UDOM
Fungua kivinjari (browser) na tembelea tovuti rasmi ya UDOM:
👉 https://application.udom.ac.tz
Utaona ukurasa wa mfumo wa maombi ya mtandaoni (Online Application System).
3. Jisajili (Create Account)
Ikiwa ni mara yako ya kwanza:
- Bonyeza sehemu iliyoandikwa “New Applicant Click Here to Register”.
- Jaza taarifa zako binafsi:
- Jina kamili
- Namba ya simu
- Password utakayotumia kuingia mfumo
Baada ya kujisajili, utatumiwa ujumbe (kwa SMS au email) wa kuthibitisha akaunti yako.
4. Ingia (Login) Katika Mfumo UDOM Application Portal
Tumia email na nenosiri ulilosajili kuingia kwenye mfumo wa UDOM Application Portal.
5. Jaza Taarifa Zako za Kitaaluma
Baada ya kuingia:
- Jaza taarifa zako za kitaaluma, kama vile namba ya mtihani wa NECTA/NACTE, mwaka wa kumaliza shule, na matokeo yako.
- Mfumo utavuta taarifa zako moja kwa moja kutoka NECTA au NACTE ikiwa umeingiza namba sahihi.
6. Chagua Kozi Unayotaka Kusoma UDOM
- Mfumo utakuruhusu kuchagua kozi hadi tatu.
- Soma maelezo ya kozi (duration, sifa za kujiunga, gharama n.k) kabla ya kuchagua.
- Chagua kozi kulingana na ufaulu wako na nia yako ya kitaaluma.
7. Lipia Ada ya Maombi UDOM
- Ada ya ku-apply kawaida ni Tsh 10,000 (inaweza kubadilika kidogo kila mwaka).
- Lipa kupitia:
- Tigo Pesa, M-Pesa, Airtel Money
- Benki kwa kutumia control number utakayopewa
- Baada ya kulipa, hakikisha unahifadhi risiti ya malipo.
8. Thibitisha na Tuma Maombi UDOM
- Kagua taarifa zako zote kuhakikisha kuwa ni sahihi.
- Bonyeza kitufe cha “Submit Application” ili kumalizia hatua ya maombi.
- Baada ya kutuma, utapokea ujumbe unaosema kuwa maombi yako yamepokelewa.
9. Fuatilia Maendeleo ya Maombi Yako UDOM
- Unaweza kuendelea kufuatilia status ya maombi yako kupitia portal ileile: application.udom.ac.tz
- Ukichaguliwa, utapokea barua ya udahili (admission letter) kupitia mfumo au email yako.
10. Baada ya Kuchaguliwa: Thibitisha Udahili UDOM
- Ukipokea majibu ya kuchaguliwa, usisahau kupitia tena kwenye portal kuthibitisha udahili wako ndani ya muda uliowekwa.
- Thibitisho hilo linaonyesha kuwa unakubali nafasi uliyopata, na ni hatua muhimu ili nafasi yako isipelekwe kwa mtu mwingine.
Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara (FAQs)
Naweza kuomba kozi zaidi ya moja?
Ndiyo. Unaruhusiwa kuomba hadi kozi tatu tofauti, lakini utapangiwa moja kulingana na sifa zako.
Vipi kama sina internet?
Unaweza kuomba msaada katika ofisi za karibu za elimu au kwenda kwenye ofisi za udahili UDOM au vituo vya huduma za maombi (help desk).
Ada ya maombi inarudishwa?
Hapana. Ada ya maombi haitarudishwa hata kama hukuchaguliwa.
Maendekezo ya Makala Zinazohusiana na UDOM Admissions
- ✔️ Sifa za Kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
- ✔️ Jinsi ya Kuthibitisha Udahili UDOM
- ✔️ Jinsi ya Ku-Apply Chuo Kikuu cha Dodoma
- ✔️ Kozi Zote Zinazotolewa na UDOM
- ✔️ Ada na Gharama za Kusoma UDOM
- ✔️ Majina ya Waliochaguliwa UDOM
- ✔️ Jinsi ya Kuomba Hosteli UDOM
- ✔️ How to Access UDOM E-Learning Portal (LMS)
Tayari umeomba UDOM? Jifunze hatua za mwisho kuthibitisha udahili wako rasmi!
Bonyeza Hapa Kujua Jinsi ya Kuthibitisha UdahiliHitimisho
Ku-apply UDOM ni mchakato wa wazi, wa kidijitali na unaowezekana kwa kila mwanafunzi mwenye sifa stahiki. Ni muhimu kufuata hatua kwa hatua kwa umakini, kuhakikisha taarifa zako zote ni sahihi, na kuomba kozi kulingana na uwezo wako wa kitaaluma. Kwa taarifa zaidi, tembelea tovuti ya UDOM au wasiliana na Ofisi ya Udahili kupitia:
Simu: +255 26 2310000
Tovuti: www.udom.ac.tz