Jinsi ya kujiunga na chuo cha Ualimu Patandi Teachers College: Ada, Fomu, Sifa na Kozi
Patandi Teachers College ni chuo kilichojipambanua kwenye kuwaandaa walimu wenye uwezo wa kuwahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum, Patandi Teachers College ni chuo kinachotoa mafunzo ya ualimu kwa ajili ya elimu maalum. Kimejikita katika kuwa kituo bora cha kuzalisha walimu wenye maarifa ya kuwahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum. Chuo kipo Tengeru, takribani kilomita 11.5 kutoka Arusha mjini.
2. Kozi Inayotolewa Patandi Teachers College
Chuo kinatoa kozi ya Stashahada ya Ualimu wa Elimu Maalumu kwa mwaka wa masomo 2025/2026. Mafunzo haya ni kwa:
- Waliohitimu kidato cha sita
- Walimu waliomaliza mafunzo ya ualimu lakini hawajapata ajira
- Walimu walioko kazini
3. Sifa za Kujiunga na Kozi Patandi Teachers College
Kwa Mwajiriwa au Asiyeajiriwa:
- Cheti cha kidato cha nne na sita (au ualimu)
- Fomu ya afya iliyojazwa na daktari wa hospitali ya serikali
- Cheti cha kuzaliwa
- Kadi ya NHIF au fedha ya bima (TSh 50,400)
Kwa Walimu Kazini:
- Barua ya ruhusa kutoka kwa mwajiri
- Kitambulisho cha kazi
4. Ada na Michango Mingine Patandi Teachers College
Ada ya Mafunzo:
- TSh 450,000/= kwa mwaka (Unaweza kulipa kwa mkupuo au kwa nusu kila muhula kupitia GePG)
Michango ya Mwaka: Patandi Teachers College
Na | Aina ya Mchango | Kiasi (TZS) |
---|---|---|
1 | Serikali ya wanachuo | 5,000 |
2 | Huduma ya kwanza | 10,000 |
3 | Usafi na mazingira | 20,000 |
4 | Usajili na kitambulisho | 20,000 |
5 | Michezo | 30,000 |
6 | Ulinzi | 30,000 |
7 | Kukodisha godoro | 10,000 |
8 | Bima ya afya (NHIF) | 50,400* |
9 | Ukarabati | 25,000 |
Jumla (bila NHIF) | 150,000 | |
Jumla (kama huna NHIF) | 200,400 |
5. Mahitaji Muhimu ya Kujiunga Patandi Teachers College
- Sare rasmi ya chuo (suti nyeusi, shati light blue, tai, na viatu vya ngozi)
- Nguo za michezo na vifaa binafsi (shuka, mto, daftari, ndoo, sahani nk.)
- Daftari ≥ 10, rimu 2, na vifaa vya mafunzo ya vitendo
- Usajili kamili unategemea uwasilishaji wa nyaraka zote muhimu
7. Maadili, Sheria na Kanuni Patandi Teachers College
Chuo kinazingatia nidhamu ya hali ya juu. Mambo kama ulevi, ujauzito, ndoa, mavazi yasiyofaa, matumizi ya madawa ya kulevya, na kutohudhuria vipindi huweza kusababisha kufukuzwa.
8. Mawasiliano ya Haraka Patandi Teachers College
- Simu ya Mkuu wa Chuo: 0767-275920 / 0716-767380
- Simu ya Msajili: 0625-991519 / 0752-355526
- Simu ya Mtaaluma: 0759-050839
- Tovuti: patanditc.ac.tz
- Barua pepe: patanditc@moe.go.tz
Soma Hii: Vyuo Vyote vya Ualimu vya Serikali na Binafsi
Hitimisho
Ikiwa unataka kuwa mwalimu mahiri wa elimu maalum, Chuo cha Patandi ni chaguo bora. Jizatiti kwa maandalizi na fuata taratibu zote kama zilivyoelekezwa katika joining instructions rasmi.