Majina Ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI na Ajira Portal 2025
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) imetoa orodha ya majina ya waombaji walioteuliwa kushiriki usaili kwa nafasi mbalimbali za kazi serikalini kupitia Ajira Portal kwa mwaka 2025. Tangazo hili linahusu waombaji waliotuma maombi yao kwa taasisi za serikali, ikiwa ni hatua muhimu kuelekea ajira katika utumishi wa umma.Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na PSRS, waombaji waliopitia mchakato wa awali na kufuzu wameitwa kwenye usaili kwa nafasi walizoomba.Orodha ya majina ya walioitwa kwenye usaili imechapishwa na inapatikana kupitia vyanzo mbalimbali vya habari.Waombaji wanaweza kuangalia majina yao kupitia:
Yaliyomo Katika Tangazo la PSRS 2025
Tangazo la PSRS linahusu:
- Majina ya waombaji walioitwa kwenye usaili.
- Tarehe na muda wa usaili.
- Aina ya usaili (waandishi au wa mdomo).
- Mahali utakapofanyika usaili.
- Maelekezo ya nini kinatakiwa kufanyika kabla ya usaili.
Jinsi ya Kuangalia Majina ya Walioitwa Kwenye Usaili
Ili kuona kama jina lako limo katika orodha ya walioitwa kwenye usaili, fuata hatua hizi:
- Tembelea Tovuti Rasmi ya PSRS:
https://www.utumishi.go.tz - Ingia kwenye Ajira Portal:
https://www.ajira.go.tz/ - Pakua PDF ya Majina:
Tafuta kiungo cha tangazo la “Walioitwa kwenye usaili Juni 2025” au “Call for Interview June 2025”. - Tumia jina lako au namba ya maombi kutafuta jina lako katika orodha.
🎧 Majina Ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI na Ajira Portal 2025
Majina Walioitwa Kwenye Usaili Utumishi (Call for Interview UTUMISHI) June 2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA BUKOBA 05-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MISSENYI 05-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MAFIA 05-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA 05-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA CHEMBA 05-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA HANANG 05-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA BABATI 04-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA 04-06-2025
- TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA (NECTA) MAJINA YA NYONGEZA 18-04-2025
Maelekezo Muhimu kwa Wasailiwa
- Fika kwenye usaili ukiwa na vyeti halisi (originals) vya taaluma na nakala zake.
- Hakikisha una kitambulisho halali kama vile NIDA au leseni ya udereva.
- Fika kwa wakati sahihi kama ilivyoelekezwa kwenye ratiba.
- Usikose kuchukua barua ya mwaliko kwenye akaunti yako ya Ajira Portal.
- Fuata masharti na taratibu zilizowekwa na taasisi husika.
Mambo ya Kuzingatia Kabla ya Usaili
- Soma vizuri tangazo na majina ili kuhakikisha unaelewa tarehe na eneo la usaili.
- Jiandae kitaaluma kulingana na nafasi uliyoiomba.
- Zingatia mavazi rasmi na mawasiliano ya heshima siku ya usaili.
- Kama kuna mabadiliko yoyote kuhusu ratiba, PSRS hutangaza kupitia tovuti yao rasmi na mitandao ya kijamii.